Thursday, June 6, 2013

TETESI ZA CRISTIANO RONALDO KURUDI MAN UNITED


Tetesi za mchezaji Cristiano Ronaldo kurejea Old Trafford zinazidi kupamba moto kila kukicha, jana zilitoka taarifa kwamba United wanajpanga kutuma ofa ya paundi millioni 65 kwa Real Madrid kwa ajili ya kumrudisha mreno huyo Theatre of Dreams. Huku pia kukiwepo na taarifa kwamba Ronaldo amekataa kuongeza mkataba na Madrid pia tayari ameiweka sokoni nyumba yake anayoishi kule Madrid sokoni.
Siku chache zilizopita mie nilipata nafasi ya kutembelea Old Trafford, wakati nikiwa OT nilipata nafasi ya kufanya mahojiano na mmoja ya wafanyakazi wa United Bwana Steve Owen kuhusiana na mambo mbalimbali yakiwemo masuala ya usajili ya wachezaji kama Rooney, Ronaldo na Bale na namna wachezaji wanavyokuwa vivutio vya biashara za klabu hiyo.


No comments:

Post a Comment